Badilisha Lugha
MRADI WA MILIONI WA AFYA YA AKILI
Kufuatilia ustawi wetu wa kiakili unaopitia mageuzi
Mradi wa Milioni wa Afya ya Akili hutumia majibu ya tathmini ya MHQ, yatolewayo bure pasipo utambulisho na hutoa ripoti kupitia barua pepe iainishayo alama na mapendekezo mahsusi.
MRADI WA MILIONI WA AFYA YA AKILI UNAKUSUDIA
- Kuunda ramani igetukayo ya ustawi wa akili kimataifa
- Kutoa maarifa kuhusiana na vichochezi vya kijamii na vya kimazingira
- Kutambua jiografia na idadi ya watu walio katika hatari
- Kuwezesha sera madhubuti na mwingiliano
Taarifa hupatikana kwa uwazi kwa jamii ya utafiti wa kitaaluma. Omba kuipata hapa.
Soma zaidi kuhusu taarifa: Seti ya Taarifa Inayobadilika ya Ustawi wa Akili wa Idadi ya Watu Ulimwenguni
RIPOTI YA HALI YA AKILI DUNIANI 2020
Ripoti ya Hali ya Akili Duniani ya 2020 inajumuisha ulinganisho wa:
- Nchi 8 zinazozungumza Kiingereza
- Mienendo ya umri, jinsia na mtindo wa maisha
- Athari zinazohusiana na UVIKO kiafya, kijamii na kifedha kwa ustawi wa akili.
Nukuu ripoti hii kama:
Newson JJ, Pastukh V, Sukhoi O, Taylor J and Thiagarajan TC, Mental State of the World 2020, Mental Health Million project, Sapien Labs, March 2021
TUSAIDIE KUTIMIZA MALENGO YETU
Mradi Wa Milioni Wa Afya Ya Akili ni harakati isiyo ya kimaslahi na tunategemea usaidizi wako utusaidie kufikia hadhira kubwa zaidi na kufanya matokeo yapatikane kwa wingi zaidi kwa umma na watunga sera.
KAMATI YA USHAURI
Mradi wa Milioni wa Afya ya Akili unasimamiwa na kamati ya ushauri ya kitaaluma ambayo hufanya maamuzi juu ya udhibiti na mifumo kuhusu faragha, mabadiliko ya mara kwa mara ya maswali yanayoweza kusaidia katika matumizi ya taarifa (kwa mfano, kama swali kuhusiana na athari za UVIKO linapaswa kuongezwa), na uamuzi kuhusiana na shabaha ya mwelekeo wa kijiografia na idadi ya watu. Kamati hiyo kwa sasa inaundwa na:
Dkt. Jennifer Newson
Mwanasayansi Mkuu, Afya ya Ufahamu na Akili, Sapien Labs USA (Mwongoza Mradi)
Dkt. Brandon Kohrt
Profesa Mshiriki wa Sayansi ya Saikolojia na Tabia, Chuo Kikuu cha George Washington, Marekani
Dkt. Helen Christenson
Mkurugenzi na Mwanasayansi Mkuu, Taasisi ya Mbwa Mweusi, Sydney Australia
Dkt. Pim Cuijpers
Profesa Kamili, Kitivo cha Sayansi ya Tabia na Mwendo, Saikolojia ya Kliniki, Chuo Kikuu cha VU Amsterdam, Uholanzi
Dkt. Eiko Fried
Profesa Msaidizi wa Saikolojia ya Kliniki, Chuo Kikuu cha Leiden, Uholanzi
Dkt. Vikram Patel
Profesa, Idara ya Afya na Idadi ya Watu Ulimwenguni, Chuo Kikuu cha Harvard, Marekani na Profesa Msaidizi na Mkurugenzi Mshiriki, Kituo cha Hali na Majeraha Sugu, Shirika la Afya ya Umma wa India, India
Dkt. Josh Seidman
Mkurugenzi Mtendaji, Kituo cha Afya Avalere Marekani